Wednesday 8 October 2008

mjadala

leo sina cha kusema ila naomba wadau muijadili picha hii kwa kadri mtavyoweza na kupenda

5 comments:

Anonymous said...

Shot imetulia ...kisiwa mtu. Mawimbi yanaipa uhai picha. Ila mmh mshikaji anaonekana na huzuni/woga wakati mazingira yanafaa kurelax.

Anonymous said...

Kutokana na somo nililopata toka ktk hii blog naweza changia jambo moja au mawili..
kwanza....mpigaji picha ilibidi asogee karibu au akate icho kipande/nafasi ya mbele ya picha kwani kwa kuacha nafasi hiyo kumesababisha taswira ya huyo jamaa na majengo kuwa mbali zaidi yaani huwezi ona uso wa huyo jamaa,na hiyo ingeweza kufanya majengo yawe karibu kidogo.Kingine naona ingebidi atumie flash ili kung'arisha hiyo picha ingawa kulikuwa na jua lakini jua lisingeathiri kitu maana lilikuwa mgongoni mwa mpigaji picha.jamani msioshe vinywa mimi sio mtaalam wa picha ila najaribu tu.

kimox said...

Mi bado sijajua alitaka kutuonesha nini katika picha hii? majengo, eneo la bahari au?Sijaona uhai katika picha

kimox.blogspot.com

Anonymous said...

Mimi nimeipenda kwa vile majengo japo yapo mbali lakini yameonekana vizuri.

maji yanaonekana kuwa ni masafi

Ila huyo mtu labda angekua focus zaidi...

Anonymous said...

Mdau asiye na utaalamu na hili.
Nilipoangalia picha hii kwa haraka haraka sikupata uhakika ujumbe wa mdau ulikuwa ni nini. Nilipoiangalia taratibu nikaona ujumbe aliotoa mdau hapo juu wa mtu kisiwa. Kwa neno moja picha inasema "Upweke". Maji, mdau an majengo vipo jirani jirani lakini vipo kivyake kila kimoja.